skills za kitaa

Tuesday, November 3, 2015

Tupia macho Video ya Justin Bieber


Tilal ya Jay -Z kuja na vichekesho


Lil Wayne kutinga na ngoma mpya


Bella:Uwezo wangu unazidikuwa mkubwa



Msanii na mmiliki wa Bendi ya Malaika Band, Christian Bella amefunguka na kusema anamshukuru Mungu uwezo wake kimuziki unazidi kuwa juu kila siku.
Msanii Christian Bella akifanya yake stejini
Christian Bella ni kati ya wasanii ambao walifanya vizuri na kuweza kukonga nyonyo za mashabiki wengi walitokea katika shoo ya Wizkid pale Leaders Club siku ya Jumamosi ya wiki iliyopita.
Akipiga stori katika kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio, Bella amesema shoo ile ilikuwa ngumu lakini aliipenda kwa sababu walipata nafasi ya kutosha kuimba kwa nafasi jambo ambalo lilifanya mashabiki waweze kusikia nyimbo nyingi zikiwa zimekamilika tofauti na shoo nyingine ambazo huwa wanaimba nyimbo nusu nusu ili kupisha wasanii wengine nao waweze kuimba.
"Shoo za wazi kama hizi huwa zinakuwa ngumu sana lakini nashukuru Mungu niliweza kufanya shoo na watu walinielewa ila niliipenda shoo kwa sababu tulikuwa tunanafasi ya kuimba nyimbo nyingi nzima bila kukata kata,” alisema Bela na kuongeza “Unajua kwenye shoo nyingi za wazi huwa tunaimba viitikio tu na sehemu maalumu za wimbo ili kupisha wasanii wengine nao waweze kuimba lakini hii imekuwa tofauti, ingawa ilikuwa ngumu kwa msanii maana ilikuwa lazima ujipange vyema kuwa na orodha ya nyimbo nzuri ili uweze kuwapa raha mashabiki na nilifanikiwa katika hilo" .
Christian Bella, Fid Q pamoja na Diamond walimsindikiza vyema Wizkid katika shoo hiyo ambapo wasanii hao waliweza kufanya shoo Live kwa kutumia bendi.

Sikiliza Madam Rita anavyozungumzia inshu za shindano lake

 Mkurugenzi wa Benchmark Production, Rita Paulsen aka Madam Rita

Belle 9 akiongelea ujio wake mpya